Kweli upendo wa mama hauna kikomo
Mama mmoja aliewalea watoto wake kwa taabu sana na wakawa
wamefanikiwa kimaisha ingawa wote walikuwa hawamkumbuki, siku moja alipatwa na
na tatizo akiwa shambani na kuvunjika miguu yote miwili.
Kwa haraka ikabidi awaombe waliokuwa wakimuuguzia nyumbani
watoe taarifa kwa vijana wake wapendwa ili waje japo kumpa fedha ili atibiwe na
kuweza kuwa mzima tena.
Baada ya kulazimishwa sana wale watoto waende kumwangalia
mama yao, mmoja wao akaamua aende ili kumaliza kelele za ndugu na wengine
kuendelea kuta bata huko walipo.
Akawasha gari yake aina ya Jeep na kwenda mpaka huko mkoani
Mbeya. Kufika pale mama alifurahi sana na kumwambia mwanawe kuwa alihitaji
msaada wake kwani bado alihitaji kufanyiwa uchunguzi zaidi ingawa alishindwa
fedha.
Yule kijana kwa dharau na jeuri aliyokuwa nayo alisema, “
mama wewe ushazeeka sasa na tatizo hili limekufanya uwe kiwete hivyo sioni haja
ya wewe kumaliza fedha kwa matibabu, bali wewe baki hapa hapa umalizie siku
zako za kuishi”
Yule kijana alimaliza na kuwasha gari akiondoka zake huku
akimwacha mama yake machozi yakimtoka na baadhi ya ndugu wamemshikilia
wakimsihi amsamehe tu Yule mtoto kwani hajui alitendalo.
Jioni ya siku ile Yule kijana akiwa ametoka bar kunywa ili akijiandae
kwa safari yake ya kurudi dar, alipatwa na ajali mbaya sana ambayo mpaka sasa
imemfanya ashindwe kutembea wala kufanya chochote kwani alivunjika mgongo.
Na kwa kuwa yeye pekee ndiye aliyekuwa akiwasaidia wenzake katika
biashara zao basi wadogo wakashindwa kusimamia biashara na mpaka hivi sasa wote
wako kijijini wakimtegemea mama yao ambaye wasamaria wema walimsaidia mpaka
anapona miguu yake.
JAMANI, Kabla hujafa hujaumbika na kumbuka upendo wa mama
hauna kikomo, kwani mama Yule aliyeambiwa kuwa ni kiwete na angekufa MAPEMA,
leohii yeye ndiye anamhudumia Yule kijana ambaye ni wakumalizia haja zote
sehemu alipo.
Na kama haitoshi wale
wanawake wazuri aliokuwa nao pamoja na marafiki wote wamemkimbiana sasa
kimbilio lake ni kwa mama yake tu.
Mkumbuke mama yako jioni hii kwa kusema “NAKUPENDA MAMA”
kama kweli unamjali
Ruksa kushare
0 comments: