Jinsi ya kufahamu kama siku ya kifo chako imekaribia

14:15:00 Unknown 0 Comments


Si rahisi kujua siku yako ya kifo, lakini kuna
watu hupata bahati ya kujua muda umefika.
Hapa ni baadhi ya mambo ambayo
yatakusaidia kujua kuwa saa yako ya kifo
imewadia…..

UTAJUA KUWA MUDA UMEFIKA..pale ambapo
majambazi wenye silaha wameteka gari lenu
wote mkaambiwa mtoe simu zenu, wewe
ukatoa NOKIA tochi na kumuhakikishia jambazi
kuwa ndio simu unayoitegemea, mara
Blacberry Bold uliyoificha kwenye chupi ikaanza
kulia

UTAJUA KUWA MUDA UMEFIKA pale ambapo
unawasha kiberiti kucheki kama kuna mafuta
kwenye jenereta iliyozima ghafla
UTAJUA KUWA MUDA UMEFIKA pale mpenzi
wako anapokwambia, “Ingia uvunguni mwa
kitanda mume/mke wangu kaja”. Wakati uko
uvunguni simu yako ya Mchina inaanza kuita"

You Might Also Like

0 comments: