MUNGU akiagiza hata shetani hufanya kama MUNGU alivyoagiza”

22:52:00 Unknown 0 Comments

Mwanamke mmoja maskini sana alipiga simu katika kipindi kimoja maarufu kilichokuwa kikirushwa na radio moja ya dini na kusema alikuwa anahitaji msaada ili apate chakula cha familia yake kwa siku hiyo.
Tajiri mmoja mwenye dharau na asiyependa kuona MUNGU akitukuzwa huku akiwa anasikiliza kile kipindi akaamua afanye kitu kwa huyu mama.
Akainakili anuani ya yule mama na kisha akampa secretary wake fedha na kuwatuma waende sokoni na kununua vitu vingi pamoja na vyakula na fedha nyingi za kumpa yule mama masikini  na akasema akiwauliza nani kaleta nyie semeni mmetumwa na shetani wa kibongo.
Baada ya kununua na kubaki na fedha kama alivyoelekezwa na tajiri, yule secretary akafika kwa yule mama na akashusha mizigo na kumpa zile fedha pia kama alivyoambiwa.
Yule mama akaipokea ile mizigo kwa furaha na kuwashukuru na kuanza kuingiza mizigo ile ndani. Secretary akamuuliza yule mama, “Je ulitaka kujua nani katutuma tuilete hii mizigo?”
Yule mama akasema, “HAPANA, Haijalishi nani kaniletea mizigo hii baada ya kusikia nikiomba kwa kupiga ile simu pale radioni, Maana MUNGU akiagiza hata shetani hufanya kama MUNGU alivyoagiza”
Unajifunza nini
Mafanikio yako ni kwa sababu ya uwepo wa nguvu za MUNGU, Hivyo Mungu daima atamalizia mipango yako na kukupa mafanikio endapo utazidi kumcha yeye na kumshirikisha katika kila kitu, haitajalisha ugumu wa jambo hilo kwa mungu kila kitu chawezekana.
Mungu atakupeleka mpaka juu ya kilele cha mafanikio na kukufungulia kitabu cha kumbukumbu ya mapito yako nasi tutajifunza kutoka kwa mafanikio yako.
Kwa sababu wewe uko nafasi ijayo kupata mafanikio mazuri kwa uweza wa “MUNGU”


Karibu Mbeya shared a link.
Posted by Fred Kihwele · 5 hours ago
205 people reached

You Might Also Like

0 comments: