Upendo wa mama haufananishwi na kitu
Siku moja jioni mtoto fuledi alimfuata mama yake jikoni akiwa ana andaa chakula cha jioni na
kumpa mama yake kajikaratasi kadogo ambako fuledi alimwandikia
Mama Fuledi alifuta mikono
yake na kukichukua kile kikaratasi ambacho kilisomeka hivi:
Kwa ajili ya kukata nyasi nakudai : TZS 5000
Kwa kusafisha chumba changu wiki hii nakudai : TZS 4000
Unavyonituma dukani nakudai : TZS 1000
Kukaa na mototo ukiondoka : TZS 2000
Kutupa takataka nakudai : TZS 3000
Kusoma kwa bidii nakudai : TZS 5000
Kusafisha sehemu ya baba kupaki gari nakudai: TZS 1500
Jumla alidai: TZS 21,500
Kwa kusafisha chumba changu wiki hii nakudai : TZS 4000
Unavyonituma dukani nakudai : TZS 1000
Kukaa na mototo ukiondoka : TZS 2000
Kutupa takataka nakudai : TZS 3000
Kusoma kwa bidii nakudai : TZS 5000
Kusafisha sehemu ya baba kupaki gari nakudai: TZS 1500
Jumla alidai: TZS 21,500
Mama akasimama pale baada ya kulisoma lile karatasi na baadae akatabasamu
na kumpokonya peni na kuandika kitu kisha akampa fuledi asome.
Mama aliandika hivi:
Kwa miezi tisa niliyo kubeba tumboni mwangu huku ukiendelea kukua:
Sitakudai
Kwa siku zote usiku ambazo sikulala kukubembeleza na kukupambia kitanda:
Sitakudai
Kwa miaka yote niliyokulea na ukanipa wakati mgumu na machozi juu yako:
Sitakudai
kwa nyakati zote za usiku ambazo sikulala nikikuuguza ili upone:
Sitakudai
kwa kila mdoli, chakula, nguo na hata kelele zako:
Sitakudai
Mwanangu Fuledi, Hata ukiongeza upendo wangu kwako:
Sitakudai
Fuledi baada ya kumaliza kusoma huku macho yakijawa na machozi
alisimama na kumwambia mama “Mama, Kutoka moyoni nakupenda.” Na kisha akachukua lile karatasi na kuandika
kwa kimombo “PAID IN FULL”.
Funzo:
·
Hutajua umuhimu wa wazazi wako mpaka utakapo kuwa mzazi.
·
Uwe mtu wa kutoa kuliko kupokea kama wafanyavyo wazazi wetu
·
Kuna mengi wazazi wametupa zaidi ya fedha.
·
BECAUSE
MONEY IS THE WORST WAYOF MEASURING HAPPINESS…♥
0 comments: