Mi sio kosa langu, wao wenyewe hawataki kabisa kula nyama ya mbwa

08:12:00 Unknown 2 Comments

Mjamaa alikwenda mji mmoja jina kapuni kumtembelea rafiki yake, chakula kikaja, akajikuta kapewa ugali na nyama nyingi na mwenyeji wake pia akapewa ugali na nyama nyingi, watoto na mke wakawa pembeni wanakula ugali na mboga za majani.

Jamaa lika mtach lakini akanyamaza akapanga wakimaliza kula amuulize rafiki yake kwa nini anafanya uchoyo huu. Walipomaliza sahani zimekwisha tolewa na baada ya kunywa maji baridiiiiiii;

JAMAA: Aise sijapenda hii tabia, sisi tumekula ugali na nyama kibao mkeo na watoto wamekula mboga za majani bila hata kipande cha nyama
MWENYEJI:Mi sio kosa langu, wao wenyewe hawataki kabisa kula nyama ya mbwa

You Might Also Like

2 comments: