Eti ikifika saa kumi na mbili kamili kitanishika tako
DOGO:"Samahani,saa hizi saa ngapi?BOUNCER:"Saa kumi na moja unusu."
DOGO:"Ok,Ikifika saa kumi na mbili kamili nitakushika tako."
BOUNCER:"Umesema nini we mtoto!"
Bouncer akaanza kumfukuza yule mtoto,baada ya mitaa miwili mtoto akaingia kwenye nyumba ya babu mmoja aliyekuwa amekaa nje anaota jua.
Bouncer nae akafika pale:
BOUNCER:"Babu nakitaka kile kitoto kilichokimbilia humu kwako."
BABU:"Kwani kuna nini unakifukuza hivyo."
BOUNCER:"Hiki kitoto kimesema eti ikifika saa kumi na mbili kamili kitanishika tako."
(Babu akaangalia saa yake)
BABU:"Sasa wasiwasi wako wa nini?....si saa kumi na mbili bado!"

0 comments: