Je, wewe ndio unaingia mjini?

19:42:00 Unknown 0 Comments

 Kwa kweli naona nichukue muda huu kutoa semina fupi kwako kuhusu mambo ya MUJINI. Kimsingi sentensi isemayo 'Mjini shule' ni ya kweli kabisa na ni muhimu kuiweka kichwani mara tu utakapoingia mjini, kwa taarifa mjini ni kuanzia Chalinze. Ok kwa leo tutaanza na sentensi ambazo asilimia 99.99 ni uwongo, na utazisikia sana. Hivyo kaa chonjo

1. ‘Kiukweli siko peke yangu, boifrend wangu yuko nje ya nchi anasoma’……hii ni sentensi ya kukufanya usimuulize inakuwaje ana maisha mazuri wakati hana kazi na na anaishi peke yake? Hapa na wewe utageuka kitega uchumi kingine, mjini utaitwa BUZI au ATM au SERIKALI na kadhalika.

2. ‘Sijichubui ni kwa sababu ya maji ya Dar es Salaam yananirudishia rangi yangu ya asili’…..hahahahahahaha hapa na cheka tu utakuwa fala kuamini mke uliemuoa mweusi anabadilika rangi kwa ajili ya maji ya bomba, ila wako wenzio wengi wanaamini rungu hili

3. ‘Nilienda Arusha kuna kakake rafiki yangu kanikopesha milioni 3 za kuanzia biashara. Lakini hakuni dai chochote’………….jiulize wewe huyo mdada ungeweza kumpa milioni 3 halafu kisitokee chochote?

4. ‘Sikupendi kwa ajili ya hela yako, I love you for who you are’…….Hii sentensi hutumika sana pia na wanasiasa ambao hudai hawataki ubunge kwa ajili ya kipato bali wanataka kusaidia wananchi teh teh teh chezea Bunge wewe

5. ‘Yule ni rafiki yangu wa kawaida tu’………hakuna kitu kama hicho hapa mjini

6. I love u too!, Ukisikia sentensi hii ina maana umeanza wewe kwa kusema I love you, na hii ni hatari kwani ina maana umeshapoteza uwezo wako wa kuwaza sawasawa. Akili imeshasiz.

You Might Also Like

0 comments: