Kama una roho mbaya usisome hapa maana utazimia
Mama mmoja baada ya kukaa kwenye ndoa kwa muda mrefu bila ya kupata mtoto huku akijaribu kila njia bila mafanikio, alingiwa na shetani na kuwa na roho ya ukatili sana.
Mama huyu akaanza kuwachukia watoto na mbaya zaidi akawachukia watoto wa jirani yake ambao walikuwa wakija pale nyumbani wanaingia moja kwa moja sebuleni na kulilia juice au hata kufungua mlango wa friji na hatimaye kuinywa juice kama wangebahatika kuiona.
Wivu wa kutokuwa na mtoto ukazidi kumfanya mama yule awe na roho ya ukatili zaidi ya shetani na kujisemesha kuwa lazima ahakikishe na majirani wanaumia kwa kukosa watoto.
Akachukua sumu na kunyunyuzia kwenye juice na kisha kuiweka kwenye friji na kuingia ndani huku akijifanya kama amelala ili wale watoto wakija kunywa wafe.
Usingizi mzito ukampitia yule mama na akaja kushtushwa na sauti ya mguno ya mtu aliyekuwa akitaabika na maumivu ya tumbo akajua kuwa sasa watoto watakuwa taabani.
Mama akajikaza kutotoka na baada ya muda akatoka nje na kushangaa kuona ni mumewe ambaye alikuwa akitapatapa baada ya kurudi kutoka kazini na kuona atulize kiu yake kwa kunywa juice bila kujua ilikuwa na sumu na kufa hapo hapo.
Funzo
Mungu wetu hujua jinsi ya kututunza sisi pamoja na mitego mibaya na hila mbalimbali tunazowekewa na mwovu shetani na vibaraka wake.
Sala
Nakuombea nawe kila aliyepanga kukufanyia baya kabla ya mwaka huu haujaisha aaibike na apate maumivu mara mbili yake.
Comment "Na iwe hivyo" kama waamini katika ulinzi wa MUNGU na kisha share
like Tabasamu na Fuledi


0 comments: