Niwape heshima iliyotukuka wanawake wooote!!!!!!!!

05:29:00 Unknown 0 Comments

Niwape heshima iliyotukuka
wanawake wooote!!!!!!!!

Imagine......

ANAKUFUMANIA:

Analia, ananyamaza, anasononeka, unambembeleza, anakuelewa,
anakusamehe - halafu anasahau.

UNAZAA NJE YA NDOA:

Anasononeka na kulia
sana. Anachukia lakini baadaye anakusamehe. Halafu analea mtoto uliyemzaa nje kwa
upendo. Kama ni kuchukiwa mtoto, si wewe uliyefanya umalaya!

UNARUDI USIKU WA MANANE UKIWA MTUNGI:

Anakukaribisha, anakuandalia chakula, unagoma kula. Anahifadhi
chakulaalichokuandalia bila manung'uniko.

UNAAMKA ASUBUHI NA MAHANGOVER:

Anakuandalia staftahi (saa nyingine unagoma kutumia staftahi yake) Unakimbilia baa kwenda kunywa Supu na kuzimua. Wala halalamiki!

CHAKULA CHA USIKU:

Ushapiga mtungi wako, unataka huduma. Unamrukia, hamna
maandalizi unamuumiza. Anavumilia ili akuridhishe. Na kesho yake tena inaweza kutokea. Hana kinyongo!

UNAJIANDAAA KWENDA KIBARUANI:

Unakuta kashakuandalia viwalo, suruali imenyooshwa kama ya askari trafik, shati limepigwa pasi ya maana! Nguo ulizovua jana zimeshalowekwa tayari kwa kufanyiwausafi! Ulichomuudhi jana
kashasahau na kukusamehe!

UNAMPA UJAUZITO:

Anauthamini, anautunza
anajifungua kwa uchungu, mtoto anakuchia wewe umpe jina, la kwakehalimo kabisa kwenye majina atakayotumia mtoto! Na pamoja na uchungu wa kuzaa, bado yuko radhi kukuzalia mtoto mwingine na mwingine tena!
Na mengine meeeenggggiiiii i sana wanafanyiwa hawa watu lakini
WANASAMEHE, WANAVUMILIA! Ni watu muhimu sana hawa watu maishani mwangu!

HIVI INGEKUWA WANAUME WANAFANYIWA HIVI INGEKUWAJE?

Kwa leo acheni tu niwape heshima zao wanawake wote:

I SALUTE AND LOVE WOMEN!

Weka tangazo bure katika blog hii Whatsapp 0713317171

You Might Also Like

0 comments: