WIVU KATIKA MAPENZI!!

13:27:00 Unknown 0 Comments

WIVU KATIKA MAPENZI!!
******************
Wivu katika mapenzi ni chachu nzuri inayoweza kufanya penzi likashamiri sana, wakati mwingine naweza kufananisha wivu na chumvi katika mboga, ila wivu ukizidi ni sawa na kuzidisha chumvi kwenye mboga.......
Watu wakiona vitu kama hivi huwa wanajenga picha zao tofauti...

- Nimekuona ulikuwa unasalimiana na Fulani huku ukimchekea!! Kucheka na mtu haimanishi una mahusiano ya kimapenzi na mtu unayewasiliana naye. lakini tahadhari ni muhimu kuchukuliwa...
- Mbona umechelewa kurudi kazini, lazima utakuwa na kimada huko kazini, mbona sio kawaida yako!
- Nani kakupigia simu saivi kwani hajui kwamba wewe ni mme/mke wa mtu. tuone namba ya huyo mtu au weka loud speaker na mimi nisikie anachoongea.
- Mbona upendo wako kwangu umepungua, tofauti na zamani, mimi nimeanza kuwa na mashaka na wewe!
- Jana nimekupigia simu umenikatia kwa nini ulikuwa na nani? mh jamani nilikuwa kwenye kikao na boss... mh kwa nini usiniambie.
HEBU MALIZIA YALE AMBAYO UNAFIKIRI HUWA YANAWEZA KUBORESHA AMA KUVUNJA UHUSIANO!!

You Might Also Like

0 comments: