Pete ya diamond yazua balaaaa
Binti mmoja ambaye aliolewa na kijana mmoja wa makamo na
ambaye alikuwa na utajiri mwingi sana,
alikuwa anategemea kupata zawadi kutoka kwa mmewe kwani alikuwa anakaribia
kuadhimisha siku yake ya kusherehekea
miaka yake ya kuzaliwa.
Kwa muda mrefu alikuwa akitamani pete moja ya almasi
iliyokuwa katika showroom moja ya duka moja maarufu sana la kuuzia vitu vya
thamani .Binti aliamini mmewe angeweza kuinunua kwani kwa utajiri wake ilikuwa
ni fedha kidogo sana. Yeye aliitamani zawadi hiyo ya pete tu na sio nyingine
kutoka kwa mmewe kipenzi.
Siku ya birthday ikawa inakaribia na yule binti akawa
anasubiri kila dalili za kuipata ile zawadi, na hatimaye siku ikafika. Asubuhi
ile yule mme akamwita mkewe chumbani mwao na akamwambia jinsi alivyokuwa na
bahati kwa kuwa na mke mzuri na mwema kama yule na jinsi alivyokuwa akimpenda kwa
dhati.
Baada ya maneno yale mme akachukua box dogo lililopambwa
vizuri na kumpa mkewe .Mkewe akiwa na hamu ya kujua nini kipo mle ndani
akaifungua bila kuchelewa na kukuta BIBLIA iliyofungwa vizuri ya yenye kava
zuri la ngozi nje yake na lenye jina
lake lilioandikwa kwa dhahabu.
Yule mke kwa hasira
akapiga kelele na kumwambia, “yaani pamoja na hela zote ulizonazo, uliona BIBLIA hii ndio zawadi ya kunipa mimi
katika siku muhimu kama hii???” kisha kwa hasira akachukua vilivyo vake na
kuamua kuondoka pale nyumbani na kwenda kuanza Maisha ake akiwa na mwane.
Miaka mingi ikapita na yule mke akawa kajiimarisha ana
nyumba yake nzuri na biashara zake na akiishi na mme mpya na familia yake wakati
yule mme wake wa zamani alikuwa keshazeeka sana. Siku moja Yule mke akaamua apange
kwenda kumtembelea mme wake wa zamani
kwani hawajawasiliana nae kwa kipindi kirefu sana tangu aondoke.
Hata kabla ya siku ya kwenda akapokea ujumbe kuwa mme wake wa zamani amekufa kwa ajali mbaya ya gari na kwa kuwa walikuwa wameoana na wana mtoto mmoja mme aliandika urithi wote uende kwa yeye na mtoto wao. Hivyo mama akaamua awahi kwenda ili akachukue mali hizo.
Hata kabla ya siku ya kwenda akapokea ujumbe kuwa mme wake wa zamani amekufa kwa ajali mbaya ya gari na kwa kuwa walikuwa wameoana na wana mtoto mmoja mme aliandika urithi wote uende kwa yeye na mtoto wao. Hivyo mama akaamua awahi kwenda ili akachukue mali hizo.
Alipowasili katika nyumba yao ya zamani, ghafla huzuni na machozi
yakaanza kumdondoka akakumbuka Maisha yao na kuamua kuzunguka vyumbani
kuangalia vitu muhimu na kuiona ile BIBLIA bado mpya kama alivyoiacha miaka mingi
iliyopita.
Huku machozi yakizidi kumtoka akaanza kuifungua ile BIBLIA
kila ukurasa na kuona mmewe aliupigia mstari
huu Matt 7:11, Ambao ulisomeka “Ikiwa
ninyi mlio waovu mnafahamu jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, ni mara
ngapi zaidi Baba yenu wa mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?”
Akiwa anaendelea kusoma kabahasha kadogo kakaanguka na
alivyofungua alilia kwa sauti kuona ni Pete ya almasi kama ile aliyoipenda
ikiwa imeandikwa jina lake na maneno kwenye bahasha NAKUPENDA MKE WNGU KIPENZI.
Ni mara ngapi tunakosa Baraka za MUNGU kwa sababu zinakuja tofauti na sisi tulivyotaka?
Funzo
Usiharibu kile ulichonancho sasa kwa kile unachokitaka
Kumbuka ulichonacho sasa pia ni moja kati ya vitu
ulivyoviomba na kuvitarajia
Daima pokea vitu kwa kusema asante hata kama ni vidogo, huwezi jua nini kipo au kitakuja kupitia hivyo
Daima pokea vitu kwa kusema asante hata kama ni vidogo, huwezi jua nini kipo au kitakuja kupitia hivyo
0 comments: