Unaumwa nini?

20:24:00 Unknown 0 Comments

Jamaa kaingia chumba cha kumngojea daktari, akakaa anangojea zamu yake, ghafla akaingia mama mmoja na kukaa karibu na jamaa;
MMAMA: Mambo?
JAMAA: Poa
MMAMA: Unaumwa nini?
JAMAA: Sehemu za siri zimeziba....haraka sana yule mama akahama na kiti. Dakika chache baadae kakaingia kabibi nako kakaa karibu na jamaa kakauliza swali lilelile kakapewa majibu yaleyale, kumbe dokta alikuwa anasikia akatoka chumbani kwake;
DOKTA: Mheshimiwa sio vizuri kujibu direct namna hiyo maswali unatisha watu, si udanganye japo useme unaumwa sikio au pua.
JAMAA: Samahani dokta, huwa sipendi uwongo, lakini nimekuelewa.....muda si mrefu kaingia polisi mmoja akakaa karibu na jamaa na kuanza mazungumzo;
POLISI: Mwenzangu unaumwa nini?
JAMAA: Masikio
POLISI: Pole sana masikio bwana yanauma sana 
JAMAA: Yangu hayaumi ila yameziba mkojo hautoki

You Might Also Like

0 comments: