Jamani huyu dada kanifanya mimi bwege sana.?
juzi nilikutana nae kwenye daladala nikaomba namba na kumwambia kuwa naomba nimtoe offer ya bia jana
Sasa mimi jana mida ya jioni nimetoka job nikaingia home kubadili mavazi ya kazi na mida ya saa moja nataka nimpigie mtoto ananiambia dia asante kwa offer nimekunywa bia hapa x bar utapitia kulipa mimi nasepa.
sasa ile bar mimi ni maarufu pale kumpigia meneja anasema ni kweli kaja dada kasema umemtuma aje anywe alikuja na rafiki zake watatu wamekunywa saint anna 4 na kuku na.chipsi.
Ndio nilimwambia tukutane pale sasa kwa nini aje na marafiki na wakati mimi sipo nakuanza kufakamia?
Kanivurugia mudi kabisa yaani, ingekuwa bar nisiyofahamika ningesema nisilipe sasa hapo nitapata aibu maana wananiheshimu sana na wanafahamu kwangu
nifanyeje marafiki? Hebu nipe mawazo yako hapa
0 comments: