SIFA NJEMA ZA MWANAUME

05:01:00 Unknown 0 Comments


1. Mpole
2. Asiwe mwepesi wa hasira
3. Mcheshi
4. Anayeshaurika
5. Anayewajali watu wa nyumbani mwake (mahitaji)
6. Aliye na shukurani na kusifu (kwa lolote jema alilolitenda mkewe)
7. Anayeaga aondokapo kwenda matembezini au kazini au popote.

10. WAJIBU WA WA MUME KWA MKEWE

1. KUPENDA - matatizo mengi hutokea kwa sababu watu hawajui maana na jinsi ya kupenda kupenda ni matendo (action) siyo kujisikia au kuhisi ni kufanya vitu vizuri kama vile kutoa, kutabasamu, kusamehe

KIONGOZI (KICHWA) MTAWALA
- Mume ni kichwa cha mke

MLINZI WA MKEWE
- Mke hujiona salama awapo na mumewe. Hivyo mume mlinde mkeo na maadui wa ndani na nje kama vile baba na mama, mashemeji/mawifi na marafik

4. KUTUNZA FAMILIA.
Kuhakiki familia inapata chakula cha kutosha, malazi, mavazi na elimu kwa watoto 

KUMPAMBA MKEWE - mume sharti ampambe mkewe apendeze ili aweze kuvutia (amununulie vipodozi, nguo nk)

KAWAIDA MWANAUME:
1. Utamheshimu mke wako kama mrithi 
2. Mke wako ni mtu wa kwanza kwako siyo ndugu zako wala rafiki zako 
4. Mara kwa mara utamwambia mke wako alivyo wa muhimu na thamani kwako 
5. Utaendelea kumpenda kwa upendo ule wa kwanza wa wakati unampata. 
6. Utakuwa kiongozi wa kusimamia nidhamu ya nyumba yako ukisaidiwa na mke wako.
7. Utakumbuka kutekeleza au kutimiza vile vitu vidogo ambavyo ulimwahidi mke wako kwamba utafanya 
8. Macho yako yataelekea kwa mke wako tu na sivinginevyo. 
9. Utafanya juhudi kusikiliza yale yaliyosemwa na mke wako. 
10. Utambusu kila siku asubuhi kwa upendo.
11. Hutakuwa mchungu likija swala la fedha.

12. WAJIBU WA MKE KWA MUMEWE KUTII
- Kutii kunakosemwa hapa ni kuwa endapo wawili mume na mke mmeshindwa kufikia uamuzi wa pamoja, basi,basi mke atatii uamuzi wa mumewe kama vile wamekubaliana awali

KULEA WATOTO (FAMILIA)
(a) Kuhakikisha afya ya mumeo na watoto
(b) Kuhakikisha kuwa chakula kinaliwa kwa wakati na kizuri
(c) Kuhakikisha usafi wa malazi, mavazi na miili yao
(d) Kufundisha watoto maneno ya Mungu
(e) Kuchunguza nyendo na tabia za watoto na mumeo na kuchukua tahadhari mapema.

KUMSHAURI MUMEO
Mke mwenye busara ni mshauri mwema kwa mumewe. Hatatoa ushauri wa kuleta maangamizi. Ushauri unafaa lakini ushauri mwingine upimwe kabla ya kufanyia kazi. 

13. ADUI WA NDOA NI:-
UTAJIRI - Tajiri hupendwa na wasichana na pia huwa na tamaa ya kutafuta fedha kiasi cha kukosa muda na mkewe

UMASKINI - kazi ya kutafuta lishe ni ya baba, hivyo hushughulika sana na kujikuta amekuwa baba zaidi kuliko kuwa mume

MADARAKA - madaraka ya ofisini huyaleta hadi nyumbanini chukuzo kwa mume/mke. Maafisa hawana muda na wake zao kwa sababu ya makongamano/semina/ziara mbalimbali.- Hivyo wake zao wengi hutumia madereva kukidhi haja zao za kimwili- Mke ambaye ni ofisa humwachia house girl kazi za kupika, kufagia chumbani, kupeleka maji bafuni na hata kutandika kitanda, hivyo kusababisha mke kupinduliwa na house girl.

You Might Also Like

0 comments: