Ukarimu pale unapogeuka kuwa TANZANITE

16:58:00 Unknown 0 Comments

Mtu mmoja aliwasili katika kijiji kimoja kilichopo kusini mwa Tanzania katika lengo la kununua ng'ombe wa kuwasafirisha kwenda kuwauza katika mikoa ya Dar, Arusha na Morogoro.

Baada ya kufika mwisho wa basi ilimlazimu kutembea zaidi ya umbali wa kilomita kumi na tano kwa miguu mpaka alipofika kijiji ambacho aliambiwa angeweza kupata ng'ombe wengi kwa kufutana na mahitaji yake.

kile kijiji hakukuwa na hotel wa nyumba ya kulala wageni zaidi ya club ya pombe za asili ambazo wenyeji wa kijiji kile walikuwa wakipata baada ya shughuli za shamba.

Akafika pale na muda huo giza lilishaanza hivyo akaongea na mama mmoja ambaye ni muuzaji wa kibanda kile cha pombe na mama akamwambia asiwe na wasiiwasi kwani atamsaidia sehemu ya kulala.

Baada ya kuridhishwa kuwa atapata sehemu ya kulala basi akala chakula na  akaendelea kunywa pombe za kienyeji na wenyeji wale huku akiwa kakaa na mzee mmoja ambaye kwa mavazi alionekana dhairi kuwa ni fukara na hutumia pombe kama njia ya kujituliza kimawazo huku akisubiri siku zake ambapo mtoa roho ataichukua roho yake na kumpunguzia maumivu ya dunia.

 Wakanywa kwa muda huku hadithi za hapa na pale zikipamba moto na mgeni akijaribu kupeleleza habari za kijiji kile ili siku ya pili biashara yake iende salama bila kokoro na amalize kazi zake na kurejea mjini kwa ajili ya biashara zake.

Mazungumzo yaliendelea mpaka akaja kujikuta kabaki yeye na yule mzee tuu na kilabu kimebaki kimya ikimaanisha hakuna aliyebakia pale zaidi yao jambo lililomfanya amhoji mwenyeji vipi huyu mama anayetuuzia atakuwa wapi?

Mzee akamjibu kuwa kashaondoka mida hii na yeye hufanya biashara mbili, hujiuza yeye na pia huuza vinywaji sasa akipata mtu wa kulala naye huwai kulala, ila kama hutajali kwa kuwa alikuahidi uende kwake basi mimi naweza kukukaribisha kwangu kama utapaweza.

wakaondoka na kwenda kwa huyo mzee ambaye yeye mke wake alifariki miaka mingi iliyopita na kumwacha na mtoto mmoja wa kiume ambaye alikua anasoma shule ya msingi wakati huo.

Wakafika na kuona kijana amesha lala na mwenyeji akatandika mkeka sebuleni na wakalala mpaka siku ya pili yake. Nyumba ilionyesha hali ya upweke na kuwa maisha hayakua mazuri.

Asubuhi wakawahi kuamka na baada ya kuamka wakaagana na kutokomea kazini baba akielekea shambani, mtoto shuleni na mgeni kusaka ng'ombe.

Jioni wakakutana na kumwacha kijana akipika chakula mgeni alichonunua na kwenda kupata pombe za kienyeji na katika maongezi ikaonyesha mgeni alifanikiwa kukusanya ng'ombe 150 na baada ya mazungumzo wakarudi waka na kulala.

Siku ya pili mgeni akakusanya pia ng'ombe 150 na siku ya tatu pia 150 jumla ikawa ng'ombe 450. Siku ya nne magari yakawasili pale na kuwabeba tayari kwa safari ya kurudi mjini.

Jioni ile ambapo siku ya pili yake alfajiri mgeni alitarajia kuondoka, wakatoka tena na kwenda kupata pombe na waliporudi mgeni aliwashukuru sana na kumwambia mzee ya kuwa kamwe hakutegemea kama angepata sehemu ambayo angeishi kwa furaha akiwa kijijini pale kama nyumba ya mzee huyo aishie na kijana wake.

Akawashukuru kwa ukarimu wao na jinsi walivyoishi kwa amani na furaha pamoja na hali zao. Akasema hana fedha za kuwapa ila anawashukuru kwa moyo wao. Akamwomba mzee azunguke kwenye bustani yake pale nje na kumuuliza kama ameona kitu, mzee akajibu hakuna kitu.

Akamwambia kesho nitaondoka asubuhi sana na baada ya kuondoka masaa mawili baadae katika hiyo bustani utaona chungu kikubwa sana na ukiufunua mfuniko utaona kitu cha ajabu usitishike wewe kichukue na kitupe pembeni na chini yake utaona vitu viwili wewe chagua kimoja tu ukichukue na ndio itakuwa zawadi yako. Mzee hakupata usingizi akiisubiri siku ya pili ifike.

Siku ya pili asubuhi yule mgeni baada ya kuondoka mzee akasubiri kwa hamu masaa mawili yapite kisha akazunguka kwenye lile shamba na kukiona kile chungu kama alivyoelekezwa na mgeni wake.

Alipofungua chungu joka kubwa likatoa kichwa chake, kwa hofu nyingi yule mzee akalishika kichwani na kulitupia pembeni nalo likatokomea vichakani.

Pale chini akaona lile joka lilikuwa limekalia kipande kikubwa cha dhahabu na kipande kikubwa cha almasi pia.Mzee yule akaichukua almasi na baada ya kupiga hatua mbili tu, chungu kile kikatoweka zake nae akaingia ndani na almasi yake na kuificha.

Siku ya pili yake mzee akajiandaa na kwenda mjini ili akaiuze ule almasi, na kwa kuwa alikuwa hana wazo la wapi kwa kuuza akaenda duka la mfanyabiashara maarufu katika mji ule mwenye asili ya kiasia na kumwonyesha kwa mashangao mkubwa yule mfayabiashara akaamua kumpa visima viwili vya mafuta na duka lake na magari ya mafuta pamoja na magari ya kutembelea na nyumba ya kuishi na mzee akakubali.

Siku chache baadae baada ya yule mzee kukabidhia zile mali zake... Akaanza kuumwa na kukaa ndani kwa miezi miwili mpaka alipokuja kupona na kuona baadhi ya mali zimeibiwa ila kwa maajabu wiki moja baaadae kila aliyeiba alivirudisha na yule mwafanya biashara akaja na kumwambia hakumtendea haki akamwongezea tena fedha nyingi.

Mpaka leo yule mzee ni mtu tajiri sana na mwanae amesoma na sasa ni msimamizi mkuu wa biashara zake na kile kijiji chake kakibadilisha na umekuwa mji mdogo wenye kila hitaji la muhimu na yeye hadi leo hajui yule mtu aliyekuja pale kijijini kununua ng'ombe alikuwa wa aina gani..............????????????

UKARIMU UNA MALIPO MAZURI

You Might Also Like

0 comments: