VITU VYA MSINGI KUZINGATIA KATIKA MAISHA YAKO

05:24:00 Unknown 0 Comments

VITU VYA MSINGI KUZINGATIA KATIKA MAISHA YAKO

1. Kuwa karibu na wazazi wako na familia yako pia

2. Kuwa makini na kila kitu katika maisha yako

3. Kuwa na kiu ya kuipenda afya yako,kufanya kazi kwa bidii, kula na kuvaaa vyema

4. Usijihusishe na mambo yasiyo na faida katika maisha yako

5. Jali thamani yako machoni mwa watu hata kama unapitia katika nyakati ngumu maishani mwako.

6. Usiuabudu umbea

7. Kuwa makini na marafiki unaowachagua kuwa nao maishani

8. Usicheze na muda kwa kuamini kesho ipo

9. Kuwa halisi wakati wa kupanga plan zako na hakikisha kila mara unazipitia kuona kama uko sahihi

10. Kuwa mwerevu kwa kuishi vyema na jamii inayokuzunguka

11. Andaa mipango inayoendana na wakati uliopo.

12. Maliza kazi zako kwa muda muafaka

13. Usilale kwa kuchelewa ukijitetea kuwa unamalizia kazi, panga muda wako kwa kufanya kila jambo kwa wakati wake

14. Hakikisha unatatua kwa busara, hekima na uvumilivu mkubwa kila tatizo linalokukabili katika maisha yako

15. Usiwe mtu wa lawama kila mara kwa wakuzungukao

16. Jitahidi kuwa mtu wa kuyakubali makosa yako na sio kumrushia mwenzako

17. Heshimu kila anayekuzunguka pamoja na changamoto zao

Weka tangazo lako bure katika blog hii

Whatsapp 0713317171

You Might Also Like

0 comments: