Hatimaye akaolewa na yule mwanaume aliyempenda kwa mika 10...........SOMA NI NZURI

12:05:00 Unknown 0 Comments



Hatimaye akaolewa na yule mwanaume aliyempenda kwa mika 10..

Mwishoni kabisa mwa tafrija fupi waliyoandaliwa na familia, mama yake alimwita pembeni na alimpa zawadi ya kitabu cha benki kilichokuwa na milioni mbili za kitanzania alizokuwa ameziweka. 

Mama akamwambia mtoto wake pekee wa kike, "Mwanangu, tafadhali chukua hiki kitabu cha benki.Kitunze kama kumbukumbu yako ya maisha ya ndoa. 

Kikitokea kitu kizuri katika maisha yenu na ambacho ukaona ni kumbukumbu basi wewe weka kiasi chochote cha fedha kwenye akaunti hii. Andika chini kitu hicho ni  nini na kiwango cha fedha ulichokiweka.

Jinsi utakavyokuwa na matukio mengi ya furaha basi kumbuka ndio hivyo hivyo na fedha zitaongezeka katika akaunti hii kwa jinsi utakavyoweka. Mimi nimekuanzia kwa kuweka fedha katika akaunti hii kutokana na tukio hili kubwa la wewe kuolewa. Matukio mengine naomba ushirikiane na mmeo kuhakikisha mnayaweka katika kumbukumbu kwa jinsi mlivyoyafurahia pamoja” 

Alipofika nyumbani akamshirikisha mmewe usiku ule alimshirikisha mmewe na wote walilifurahia jambo lile na kuona ni wazo jema sana. Kitabu chao cha benki kilionekana hivi baada ya miezi michache…

- February 7 – 200,000: Kumbukumbu yake ya kwanza ya siku ya kuzaliwa baada ya ndoa
- March 1 – 600,000: Aliongezewa msharaha kazini
- March 20 – 400,000: Shukrani ya kurudi salama kutoka mapumzikoni Kilolo
- April 15 – 4,000,000: Ana ujauzito!
- June 1 – 2,000,000: Alipandisha cheo na kuwa meneja kazini kwake

Mambo yaliendelea kuwa hivi kila tukio lilipojitokeza lenye furaha...

Ingawaje, miaka ilivyozidi kuyoyoma wakajikuta wakianza kupigana na kupigizana kelele kila kukicha.Hawakuongea tena sana kama hapo awali, kila muda walijilaumu kuoana na ule upendo wa awali ukatoweka kabisa.

Siku moja mke akampigia simu mama yake na kumwambia, "Mama, hatuwezi kuendelea na ndoa hii. Tumeamua kupeana talaka. Nashindwa kuamini nini kilinikuta nikaona na huyu mwanaume!”

Mama akamjibu, "Fanya lolote utakalo mwanangu,kama ni kweli umeshindwa kuvumilia. Ila kabla ya kufikia uamuzi huo kuna kitu naomba ukifanye kwanza.Unakumbuka kile kitabu cha benki nilichokupa wakati wa harusi yako? Tafadhali naomba ukachukue fedha zote na uzitumie kwani hutakiwi tena kuwa na kumbukumbu za maisha ya ndoa ambayo yana mwisho mbaya kama huo wako."

MKe alikubaliana na mama yake na akaenda siku ya pili yake benki wakati huu alikuwa kwenye mstari akisubiri nafasi yake ili akatoe fedha zote na kuifunga akaunti ile. Akiwa pale kwemye mstari anaisubiri zamu yake akaona achukue kile kitabu na kuangalia kumbukumbu za matukio yao ya furaha na kiasi cha pesa kilichowekwa. 

Aliangalia tena na tena kwa muda kisha zile kumbukumbu za yale matukio yote yenye furaha zikamrudia. Wakati huo macho yake yakawa yamejawa na machozi hivyo akaamua kurudi nyumbani. 

Aliporudi nyumbani akampa mmewe kile kitabu na kumwambia mmewe akazitumie zile fedha zote kabla ya wao kupeana talaka.

Siku ya pili mme akawasili benki, na tukio lililomtokea mkewe jana yake likamtokea pia mmewe. Alizidiwa pia na furaha ya matukio mazuri nay a kumbukumbu aliyoyafanya na mkewe katika kipindi cha ndoa yao na kumfanya arudi nyumbani machozi yakiwa yanamlengalenga.

Alipofika nyumbani akampa kitabu mkewe na kulikuwa kuwa fedha mpya imeingizwa katika akaunti hiyo (5,000,000) ikiwa na maneno, “Leo ndio siku ambayo nimegundua kuwa nakupenda sana mke wangu katika miaka yote tuliyokaa pamoja na jinsi ulivyonipa furaha katika maisha haya”

Wakakumbatiana na kulia kwa pamoja.KItabu chao kikarudisha katika sanduku lao maalumu na kuendelea kutunzwa huko

AMKA TOKA NDOTONI MAPENZI KAMA HAYA HAKUNA WEWE ENDELEA KUOTA TUU

Ila share

You Might Also Like

0 comments: