jamaa akaanza kulia

11:10:00 Unknown 0 Comments

Jamaa alioa kwa furaha nyingi na vifijo na hatimae kuanza kuendelea na maisha yake. Lakini hata wiki mbili hazikupita ndoa ikaanza kuwa chungu maana kila alipokuwa nyumbani mke alikuwa anataka. Asubuhi, mchana, jioni mke alikuwa anadai haki yake, jamaa alikuwa kachoka kabisa kabisa, hata kazini akawa hana raha. Na mke akamwambia kuwa anataka mtoto na mchakamchaka utaendelea mpaka mtoto apatikane. Hatimae jamaa alifikia wakati hata jongoo akaacha kupanda mtungi, nyumbani pakawa hapakaliki. Akamwambia rafiki yake aliyempeleka kwa mganga mmoja;
MGANGA: Hili tatizo lako nilikuwa na dawa yake lakini imeisha imebaki kidogo itakayotosha jongoo kusimama mara tatu tu.
JAMAA: Hata hiyo itatosha mzee nyumbani kumekuwa jehanamu.
MGANGA:(Akatoa unga fulani) Huu paka sasa hivi kwenye jongoo, baada ya hapo ukitaka kutumia jongoo sema tu BRAAAAAAM atasimama, ukitaka atulie sema BRAAAAM BRAAAAAAM......jamaa akapaka ule unga akaona ajaribu
JAMAA: BRAAAAAAAM loh hatari kubwa kidogo vifungo vya lisani vifunguke, jamaa akafurahi sana. BRAAAAAM BRAAAAM jongoo akatulia, akaingia kwenye gari lake kuwahi home, akajua ana mara mbili zimebaki. Akasimama kwenye traffic lights, si ikaja pikipiki ikapiga BRAAAAAAAAM, jongoo kainuka, jamaa kachanganyikiwa, kabla hajafanya lolote pikipiki ikalia BRAAAAM BRAAAAM ikaondoka na jongoo akatulia. Jamaa akawahi home akijua imebakia nafasi moja tu. Akaingia kwake akaoga vizuri akamuita mkewe;
JAMAA: Mke wangu njoo, (mke alipoingia tu), BRAAAAAAAM
MKE: Hakuna cha BRAAAAAM BRAAAAM nataka haki yangu...........jamaa akaanza kulia

You Might Also Like

0 comments: