nikatoka kwangu spidi huku navaa nguo

10:54:00 Unknown 0 Comments

Baunsa wa night club alienda kutibiwa kutokana na maumivu makali baada ya kupata mshtuko wa mgongo;
DOKTA: Umeumiaje?
BAUNSA:Nilipoingia nyumbani kwangu leo asubuhi, nilipata hisia kuwa mke wangu ana mtu chumbani kwetu,nikaingia chumbani kikomandoo nikamkuta mke wangu peke yake,mara nikasikia mlango wa sebuleni umefunguliwa kwafujo, nilipochungulia dirishani nikamwona mtu anakimbia huku anavaa shati, nikachukua fridge nikamrushia nikiwa ghorofa ya tatu,hapo ndipo niliposhtua uti wa mgongo.....Alipomaliza tu kauli yake,akaingia mgonjwa
mwingine kaharibika kama kagongwa na gari.

DOKTA: Vipi ndugu,nini kimekusibu?
MGONJWA:Nilisahau kuweka alarm asubuhi nikachelewa kuamka kwenda kazini, kazi yenyewe ndio kwanza nimeanza baada ya kukaa jobless kwa muda mrefu, nikatoka kwangu spidi huku navaa nguo, mara nikapondwa na fridge kichwani.

You Might Also Like

0 comments: