Ohoo masikini umemeza
Siku ya harusi ilikuwa inakaribia,
lakini bwana harusi na bibi
harusi wote walikuwa natatizo
kubwa sana la siri, kila mmoja kichwa
kinamuuma itakuwaje ndoa
ikiianza. Bwana harusi akaenda kwa baba yake;
BWANA HARUSI: Baba ninatatizo nitafanyaje?
BABA: Tatizo gani mwanangu?
BWANA HARUSI: Baba nina
tatizo miguu yangu inanuka sana si mke atanikimbia baada ya wiki
BABA: Uwe unaosha mara kwa mara harufu itatoka
BWANA HARUSI:Baba hujui,harufu ni mbaya sana
BABA: Basi uwe unavaa soksi daima...jamaa akaona hili linaweza
likanasaidia. Bibi harusi akaenda kwa mama yake;
BIHARUSI: Mama nina tatizo kubwa nikiamka asubuhi mdomo
wangu unanuka mme atanikimbia
MAMA: Kila mtu akiamka asubuhi mdomo unanuka hilo si tatizo.
BIHARUSI: Mama huelewi domo langu linanuka unaweza
kufikiri panya kafa
MAMA: Basi ukiamka asubuhi usifungue mdomo mpaka upige mswaki kwanza...
.Wapen zi hawa wakaoana na kila mmoja akashilia ushauri mambo
yakawa powa.Siku moja baada ya miezi mitatu, mume aliamka asubuhi
akagundua soksi moja imevuka, akahangaika awahi
kuipata kabla mkewe hajaamka, bahati mbaya
mke akaamka;
MUME: Samahani umenionea
soksi?
MKE: Hapana,......ma ra harufu
mbaya ikaenea,
MUME: Ohoo masikini umemeza
soksi yangu....


0 comments: