heeeeeeeee kumbe watu ndio wako hivi????? Duh
Mambo ya ajabu ajabu usiyoyajua kuhusu binadamu
Wakati wewe unatoa mimba, kuna mtu anasaka mimba kwa miaka kumi na zaidi bila mafanikio
Wakati wewe kijana una mkataa binti uliyempa mimba, kuna mzee ana miaka nenda rudi akiwa anakesha akiomba Mungu amjalie mtoto
Wakati wewe una inyanyasa familia yako leo, kumbuka kuna mtu anatamani apewe familia na aipende
Wakati wewe unaichukia kazi uliyonayo, kuna mtu ana vyeti vyake safi ila hajawahi kupata kazi ya aina yoyoye na anaishia kwenye interview tuu
Wakati wewe unaichukia nyumba unayoishi sasa, kuna watu hawana sehemu ya kulala usiku wa leo
wakati wewe unakula na klusaza chakula na kumwaga kuna mtu leo hana uhakika wa kula
Wakati binadamu wengine wanafurahia kuua kuna watu wanahangaika kuhakikisha wanajaribu kuokoa maisha ya ndugu zao bila mafanikio
Wakati wewe humshukuru Mungu kwa uhai ulionao, kuna mtu ni mwaka wa nne sasa naumwa na yupo kitandani hajui ni lini atatoka ndani mwake akiwa mzima
Wakati wewe unawadharau na kuwasahau wazazi wako bila kuwajali. Kuna watu wanalia usiku kucha na kuumia kuwakosa wazazi
Wakati wewe ni bingwa wa kupoteza marafiki kwa ubinafsi wako kuna watu walia pamoja na fedha na mali walizonazo ila hawana marafiki wa kukaa nao na kuwashauri
Kumbuka, hakuna maisha yoyote zaidi ya haya na huna budi kuwa na shukrani kwa kile unachojaliwa sasa....
Pia ni bora kuwa na mpangilio wa maisha ukimtanguliza MUNGU na
kushukuru kila ulichonacho na kufurahia nyakati ulizonazo
Soma maoni ya wadau kwa kubofya HAPA


0 comments: