Umasikini sio sababu ya kuwa mchafu wala utajiri Sio kuwa na kila kitu hata kama hukihitaji

05:57:00 Unknown 0 Comments

Umasikini sio sababu ya kuwa mchafu wala utajiri Sio kuwa na kila kitu hata kama hukihitaji. Hebu angalia hapo nyumbani kwako!

Vitu msivyovihitaji Leo wala kesho
mmeweka vya nini? Umenunua makochi mapya Yale ya zamani mmegawana vyumbani mnaishia kurundika minguo hapo na kufuga
mipanya, godoro umenunua jipya la zamani umeviringisha juu ya kabati, kabatini kwako kuna nguo ulivaa ukiwaona secondary mpk
Leo unazo eti ukumbusho au utazivaa ukipungua, jikoni ndo shida iliposhika hatamu !!

Mivyombo ya plastiki imepaukiana
imeyayuka na moto ipo tu eti vyombo vya watoto,mahotpot yamekata roho imebaki kuwa
sufuria we unalo tuu, ndoo hata hazitumiki zipozipo tu hata maua hazifai kupandia we unazogo tu huchomi,hutupi wala huzihitaji,
vyombo vya udongo fina mapengo na magego km vinang'atwaga na kila kimoja na dizaini yake havifanani coz set imeshavunjikavunjika
hivo ndo vimebaki,Dressingtable imejaa mikopo na mibox haina Kazi,perfume ya mwaka 2000 unayo hapo kisa ukumbusho wa
zawadi,stoo yenu wenyewe ila mwaiogopa kuingia coz imejaa vitu visivyohitajika imekuwa
ghetto la panya badala Ukiweka mnavyohitaji, nje ya nyumba kuna gari la urithi la babu lipogo tu hapo linafuga ndege,kutupa vitu
visivyohitajika hamtupi eti Dhambi na kugawa hamgani coz mmeviharibu hadi mwisho mtampa nani?

Kutwa mnapishana mahospiitalini mnaumwa flu na vifua kila
siku,kimoja Kwann msiumwe na mnakaa dampo ?

Hivi mnajua km huu ni ugonjwa?
Unaitwa hoarder disorder. Tena
mnawaambukiza wanenu as wanajua kwao hata kikopo cha icecream hakitupwagi kinaoshwa kinawekwa hapo. Halafu bado
unaendelea kumuomba Mungu akupe, akupe uweke wapi na kwako pameshajaa?

Credit: Joseph Mwaisango

You Might Also Like

0 comments: