DADA ZANGU NI VIZURI KAMA MKIYAFAHAMU HAYA.!

17:27:00 Unknown 0 Comments

✅DADA ZANGU NI VIZURI KAMA MKIYAFAHAMU HAYA.!👍🏾💕

👉 Mwili wako sio Maonesho, kila
mwanaume auone.

👉 Mwili wako sio Mdoli kila mwanaume Auchezee.

👉 Mwili wako sio dampo, upokee kila
uchafu wa mwanaume.

👉 Mwili wako sio Mali ya umma kila
mwanaume akutumie.

👉 Mwili wako sio kiburudisho, kila
mwanaume Ajiridhishe.

👉 Mwili wako sio pazia la Sebuleni,
kila mwanaume Akufunue.

👉 Mwili wako sio karanga za
kutembezwa mtaani kila mwanaume
Akuonje Utamu wako.

🔹 Mwili wako ni wa Thamani sana.
Mwili wako ndio utu wako.

🔹 Ebu Tunza Mwili wako nao
Ukutunze. Uheshimu Mwili wako nao
Utakuheshimisha.

🔹 Si kila mtu wa kuushika Mwili
wako. Usitumie Mwili wako kama
kitegauchumi, Usitumie Mwili wako
kama dhamana ya kupata vile
unavyohitaji.

🔹 Usitumie Mwili wako kama Njia ya
kupata Mume Atakayekuoa. Kama
Mungu amepanga Uolewe utaolewa tu
dada yangu hata bila ya kufunua Sketi
yako. Muamini Mungu Yeye ndiye
aliyeshikilia maisha yako.

🔹 Kuna mtu mmoja tu anayestahili
kuugusa Mwili wako, kuuona Mwili
wako, kuujua Uzuri wako.. Msubiri,
Usiwe na Haraka, Mungu atamleta
kwako. Endelea Kusubiri.

🔹 JITUNZE, JITHAMINI, JIKUBALI NA
JIAMINI..!👍🏾💕

You Might Also Like

0 comments: