wali Je, nimshtue Mchungaji au ndio muujiza alioniombea umetokea?

21:39:00 Unknown 0 Comments

NILIKUWA nimeishiwa sana njaa inaniuma kwa bahati nikakutana na mchungaji wangu mtaani. Nikamueleza tatizo langu na kumuomba japo alfu mbili nikanunue chips mayai.

Kwa masikitiko makubwa mchungaji akanambia hana hata senti au lazima angenisaidia mimi mwanakondoo wake, lakini akaniwekea mikono kichwani na kuniombea Mungu afanye muujiza nipate pesa ya kula.

Alipomaliza kuniombea wakati anaondoka akatoa kitambaa mfukoni ajifute jasho, na pale pale noti ya shilingi alfu kumi ikadondoka Mchungaji hakuiona akaendelea na safari.

Swali Je, nimshtue Mchungaji au ndio muujiza alioniombea umetokea?

Soma pia kupitia HAPA

You Might Also Like

0 comments: