Siku moja Fuledi akiwa mdogo
sana aliitengeneza kadi kwa kutumia mikono na kuwapa wazazi wake…..
Katika
ile kadi yake ndogo ndani yake ikiwa na picha nzuri aliandika maneno haya ….. “kuna
wakati nawaudhi wazazi wangu kwa kuwa ni mdogo na nina andika andika ukutani–
Ila
ninakua kila siku– na kuna siku haya maandishi yangu ukutani yatapotea kabisa
na mimi nitakuwa mtu mzima ….hivyo ninaandika maneno haya leo kwa kutumia kadi
hii ili muweze kuyaweka katika kumbukumbu zenu– na kwa uhakika
mkumbuke maandishi yangu yalikuaje nikiwa mtoto mdogo”……
Funzo
Usisite
kutumia muda wako kukaa na watoto wakati mambo yako hayapo sawa au mpaka upate
fedha nyingi sana au mwaka ujao ukiwa huru na kazi zako za kiofisi na una muda
mwingi” …
Kama
huta yafanya Maisha yako kuwa ya furaha kwako, Maisha yatakufanya usiwe na
furaha, kwani Maisha hutufanya tuwe na tabia za ubinafsi kwetu ….
Zawadi kubwa uliyonayo kwa
wanao ni nafasi ya muda wako kwa ajili yao …


0 comments: