SIFA NJEMA ZA MWANAMKE

04:58:00 Unknown 0 Comments


1. Awe mwema 
2. Mwenye hekima
3. Mwenye adabu
4. Mwenye busara
5. Awe mkarimu
6. Msafi (mwili na nyumba)
7. Mpole
8. Mwenye huruma
9. Mdadisi
10. Mvumilivu
11. Mcheshi (kiasi)Yampasa mke aanze siku kwa kauli nzuri hata kama anaumwa:-- Amsalimie mume

- Amwage mumewe akimtakia kazi njema baada ya kumuandalia
(a) Maji ya kuoga
(b) Kifungua kinywa
(c) Nguo za kuvaa siku hiyo

Mume atokapo kazini:-
(a) Mkaribishe kwa tabasamu, mkaribishe kwa furaha.
(b) Mpigipige mgongoni
(c) Vaa nguo nzuri (mwanaume hupenda anachoona) macho huvutiwa kwa kuona
(d) Waeleze watoto wako unavyompenda baba yao ( watoto nao watawapenda wote)
(e) Kila mmoja wenu ajue kile anachopenda ua anachotaka

ILI KUMHESHIMU MUME
1. Muombee kila siku - Yeye alivyo hekima, busara, ulinzi, baraka, ujuzi, uelewa, kiroho, mafanikio, kushinda majaribu nk - angalia na tarajia majibu ya maombi - Mshukuru Mungu kwa kazi anayofanya kwa familia yako - Mshukuru Mungu kwa ajili ya Mume wako- ombea mtazamo wako.
2. Kumbuka Mungu amemuweka mume wako kuwa kiongozi wa nyumba yako pamoja na wewe.
3. Angalia sifa za mumeo na uzikubali na ongeza mara kwa mara
4. Mwambie mumeo ni namna gani unamfurahia na kumpenda
5. Usitoe sifa zake mbaya mbele za watu au kubisha
6. Mtie moyo na kuwa msaaada wakati wa jambo gumuJihadhari na jinsi unavyomuuliza maswali
7. Changamkia pale anapoonesha upendo
8. Fikiria mambo mazuri juu ya mumeo
9. Thamini vitu anavyovipenda na asivyovipenda Mith 12:4

KAWAIDA MWANAMKE

1. Usitegemee starehe nyingi kama zile ulizokuwa unapata kwa wazazi wako au ndugu zako
2. Utakuwa na juhudi katika kujenga nyumba ya mume wako uliye naye.
3. Hutakuwa mgomvi na mchokozi wala kumpiga mumeo kwa mwiko
4. Utampa mume wako haki yake
5. Thamani ya mumeo ni zaidi ya wanaume wote. 
6. Umtii mumeo kwa Roho ya upole na unyenyekevu
7. Usimuruhusu mtu yeyote atambue kwamba unao wakati mgumu ( siri za ndani zisitoke nje) 
8. Utahaakikisha macho yako yanamwangalia mumeo wakati amevaa kabla ya kutoka kwenda kazini au kutembea
9. Utajitoa na kumtii mumeo kwa moyo wote na kumruhusu kuwa kichwa cha nyumba
10. Utahakikisha mumeo ni bora kuliko watu wengine
11. Mwanaume ni dereva wa gari la ndoa na mwanamke anaweza akashauri na kupednekeza njia ya kupita na siyo kunyang'anya usukani 

You Might Also Like

0 comments: