HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU " Season 5

15:42:00 Unknown 0 Comments

HADITHI KALI NA YA KUSISIMUA "SIMU YA AJABU "

Season 5

ILIPOISHIA JANA

Nilinyanyuka haraka na kuelekea usawa wa ziwa bila kujua naelekea wapi? Mara ghafla nikashtishwa ba sauti ya mwanangu akisema baba na mimi nije kuogelea?

Ile nageuka tu nilichokiona...................................... Fuatilia kisa hiki kesho mida kama hii

Soma mwendelezo wake

ILE nageuka tu nilichokiona kilinifanya nibadilishishe uamuzi wa kuelekea ziwani kwani alikuwa mke wangu akiwa na mwanetu mdogo.

Akaniita na kuniuliza, " mbona umenyanyuka haraka na kuelekea ziwani?"

"Nimepata mzuka wa kwenda kuchezea maji mama watoto" nikamjibu huku nikichezea maji ingawa kichwani mwangu akili iliniruka wakati huo.Basi nikageuza na kuelekea upande aliokuwepo.

Ilipofika saa tatu usiku huku kichwa changu kikiwa na mawazo tele juu ya simu itakayopigwa na hamu ya kula ikiwa imenitoka na baadhi ya vyakula vikinikodoea macho nilijiuliza.

Mimi wa kunywa bia moja saa zima? Kweli mawazo yamenishika.
Muda wote nilikuwa nikiitazama simu ili kuona nini kitajiri.

Muda ulizidi kwenda na ile bia ikanizia na hatimaye kuyafumba macho yangu kwa usingizi mzito.

Asubuhi nililipoamka nikakuta missed call zaidi ya 10 na meseji moja kutoka kwenye ile namba.

Kwa kweli nilitamani nisingeamka na kuelendea na usingizi ulionifariji sana.

Wazo likanijia kichwani "haya mambo nimshirikishe mke wangu?"
Nikaona nijikaze kiume na kutoka kwenda bafuni kuoga bila kuifungua ile meseji.

Bafuni nilikaa zaidi saa moja nikiitafakari ile meseji itakuwa ina nitaka nini mimi?

Niliporudi toka bafuni nikaitazama ile simu juu ya kitanda ila wakati huu nikaifungua chupa yangu ya pombe kali aina ya grants na kuigigida ili kujiongezea ujasiri.

Nikaitazama ile simu ambayo ilikuwa muda huo kiganjani kwangu kisha nikaufungua ule ujumbe.

Jumbe uliandikwa hivi, " acha kuendekeza pombe wewe wanaume, pombe sio chai ambayo utakunywa na maandazi ili kutatua matatizo yako kuwa wanaume wewe!!"

Duuh!!! Hakuishia hapo mstari ulionichosha zaidi ni huu uliosema hivi, " nitakupigia baadae sasa leo zima simu uone!"

Dakaika kama tatu hivi wakati na itafakari hiyo sms nilisikia kelele toka nje. Nilipotoka nje nilimwona mke wangu alikuwa akiniita huku akilia kwa sauti ya kuchanganyikiwa.

Mtoto wetu alidumbukia kwenye maji na kwa bahati nzuri aliweza kuokoka baada ya mramaria mwema kumwokoa.Hivyo basi tukaelekea hospitali kupata matibabu zaidi.

Ilipofila mida ya saa kumi jioni tukiendelea kumwangalia mwanetu nilipokea ujumbe mwingine.

Kwa kuwa nikikuwa na stress za mwanangu niliufungua ule ujumbe bila kufohia na kuusoma.

Ujumbe ule lisema, " pole baba na mjukuu, manaendeleaje mbona simu yako haipokelewi?"

Duuuuuh, nilishusha pumzi ndefu baada ya kungundua ujumbe ule ulikuwa wa mama.Nilipomaliza kuusoma ule ujumbe nikairudisha ile simu na kuelekea wodini kumwangalia mtoto na kumwambia mke wangu juu ya ujumbe ule.

Tukaruhusiwa muda mfupi baadae na kuelekea hotelini ambako tulipofika hotelini mhudumu wa hotel aliniita na kuniambia kuwa nina ujumbe wangu.

Ujumbe huo ulitoka kwenye namba ilele na baada ya kuzisoma zile namba nikagundua ni namba ile ile ambayo hunipigia

Ujumbe ule ulisema hivi, .....................................................

Ujumbe huo ulisema nini? Usikose mwendelezo wake kesho muda kM

Itaendelea kesho muda kama huu

Nakutakia jioni njema

Share kama umeipenda

Maoni whatsapp 0713317171

You Might Also Like

0 comments: